Psalms 35

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

(Zaburi Ya Daudi)


1 aEe Bwana, pingana na wale wanaopingana nami,
upigane na hao wanaopigana nami.

2 bChukua ngao na kigao.
Inuka unisaidie.

3 Inua mkuki wako na fumo
Fumo ni sawa na sagai, maana yake ni mkuki mfupi.
lako
dhidi ya hao wanaonifuatia.
Iambie nafsi yangu,
“Mimi ni wokovu wako.”


4 dWafedheheshwe na waaibishwe
wale wanaotafuta uhai wangu.
Wanaofanya shauri kuniangamiza
warudishwe nyuma kwa hofu.

5 eWawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,
malaika wa Bwana akiwafukuza.

6 Njia yao na iwe giza na ya utelezi,
malaika wa Bwana akiwafuatilia.

7 fKwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,
na bila sababu wamenichimbia shimo,

8 gmaafa na yawapate ghafula:
wavu walionifichia na uwatege wenyewe,
na waanguke katika shimo hilo,
kwa maangamizo yao.

9 hNdipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana
na kuufurahia wokovu wake.

10 iNitapaza sauti yangu nikisema,
“Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana?
Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao,
maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyang’anya!”


11 jMashahidi wakatili wanainuka,
wananiuliza mambo nisiyoyajua.

12 kWananilipa baya kwa jema
na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

13 lLakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia
na nikajinyenyekesha kwa kufunga.
Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

14 mniliendelea kuomboleza
kama vile wao ni rafiki au ndugu.
Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni
kama ninayemwombolezea mama yangu.

15 nLakini nilipojikwaa,
walikusanyika kwa shangwe;
washambuliaji walijikusanya dhidi yangu
bila mimi kujua.
Walinisingizia pasipo kukoma.

16 oKama watu wasiomcha Mungu wamedhihaki,
wamenisagia meno.

17 pEe Bwana, utatazama mpaka lini?
Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,
uhai wangu wa thamani
kutokana na simba hawa.

18 qNami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,
nitakusifu katikati ya watu wengi.


19 rUsiwaache wale wanaonisimanga,
wale ambao ni adui zangu bila sababu;
usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu
wakonyeze jicho kwa hila.

20 sHawazungumzi kwa amani,
bali wanatunga mashtaka ya uongo
dhidi ya wale wanaoishi
kwa utulivu katika nchi.

21 tHunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha!
Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”


22 uEe Bwana, umeona hili, usiwe kimya.
Usiwe mbali nami, Ee Bwana.

23 vAmka, inuka unitetee!
Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.

24 wNihukumu kwa haki yako, Ee Bwana Mwenyezi Mungu wangu,
sawasawa na haki yako;
usiwaache wakusimange.

25 xUsiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!”
Au waseme, “Tumemmeza.”


26 yWote wanaofurahia dhiki yangu
waaibishwe na wachanganyikiwe;
hao wanaojiinua dhidi yangu
wavikwe aibu na dharau.

27 zWale wanaofurahia hukumu yangu ya haki
wapige kelele za shangwe na furaha;
hebu waseme siku zote, “Bwana atukuzwe,
ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”

28 aaUlimi wangu utanena haki yako
na sifa zako mchana kutwa.
Copyright information for SwhKC